Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile
Wakili.tv

@wakilitv

WAKILI TV : Televisheni ya Mtandaoni inayomilikiwa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kwa Malengo ya kutoa Elimu ya Kisheria

ID: 1263386315976040448

linkhttps://www.youtube.com/channel/UC5uwTzHaVDN-eHSqxD4zx9Q calendar_today21-05-2020 08:29:48

810 Tweet

1,1K Followers

163 Following

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Rais wa TLS wakili Boniface Mwabukusi amehoji waziri wa mambo ya ndani, Innocent Bashungwa kuingilia mhimili wa mahakama na kama tabia hiyo ya kuingiliwa mhimili huo ikiendelea kama mawakili wataweka kalamu chini kushinikiza mihimili kutokuingiliana.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Tamko la Chama cha Wanasheria Tanganyika juu ya shambulio la Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) Padre Charles Kitima.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema wapo baadhi ya watu wanahusisha tukio hilo kwamba serikali imefurahi juu ya shambulio la Padri Kitima jambo ambalo halina ukweli.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Tupo tayari kukuletea matangazo ya moja kwa moja ya Kongamano la Kitaifa Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa Mwaka 2025 kutoka makao makuu ya TLS jijini Dar es Salaam. Tufuatilie kupitia Youtube chaneli ya Wakili TV.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,imekataa ombi la upande wa mashitaka la kutaka kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA,Tundu Lissu,ya kuchapisha taarifa za uongo isikilizwe kwa njia ya mtandao,na badala yake imekubaliana na hoja ya upande wa utetezi uliotaka afikishwe mahakamani.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

TLS ina jukumu la shangazi kuna wakati itakusema ukinuna unune, ila shangazi atasema tu, atakemea, atafinya kidogo lakini mwisho wa siku shangazi hakuchukii - Boniface Mwabukusi

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Jaji Mstaafu Robert Makaramba ametoa ufafanuzi kuhusu suala la kiapo. Amesema hayo wakati wa mjadala wa mkutano mkuu wa Chama cha Wanasheria Tanganyika uliofanyika tarehe 8 Mei 2025 ukumbi wa AICC jijini Arusha. #TLSAGM2025

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Kiapo hakiondoi 'Conficts of interest' - Rais Mstaafu wa Tanganyika Law Society(TLS) wakili fatma karume aka Shangazi . Amesema hayo wakati wa mjadala wa mkutano mkuu wa Chama cha Wanasheria Tanganyika uliofanyika tarehe 8 Mei 2025 ukumbi wa AICC jijini Arusha. #tlsagm2025

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene amesema kipindi cha uchaguzi huwa wanakanyagana sana ndani ya CCM kuliko nje ya CCM. Amesema hayo wakati wa ufnguzi wa Mkutano wa TLS jijini Arusha. #tlsagm2025

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro amesema serikali itaendelea kushirikiana na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kuhakikisha huduma ya msaada wa kisheria inakua endelevu kwa wananchi.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa ametolea ufafanuzi uwepo wa taarifa za upotoshaji uliojitokeza Mei 20,2025 kupitia baadhi ya akaunti za mitandao ya kijamii, kwa kuchapisha maudhui yenye lengo la kuzua taharuki kwa wananchi. Ufafanuzi umefanyika Mei 21, 2025 Jijini Dodoma.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Waziri Gwajima amesema hadi kufikia mwezi Aprili mwaka huu, migogoro ya ndoa 97,234 ilikuwa imepokelewa kupitia Kitengo cha Ustawi wa Jamii katika ngazi ya halmashari na Taifa ambapo kati ya hiyo, 81,820 ilipatiwa ufumbuzi na 15,414 ilipelekwa mahakamani kwa hatua zaidi.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Je wafahamu kuwa Dalali haruhusiwi katika sheria ya Ardhi? Wananchi wengi huwatumia Madalali katika mchakato wa ununuzi wa viwanja na umiliki wa ardhi bila kufahamu taratibu za kisheria. Tembelea Channel ya Wakili Tv kupata elimu zaidi juu ya masuala mazima ya umiliki wa ardhi.

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Wakili wa kujitegemea Edwin Mugambila amefafanua mamlaka za Rais wa nchi kuteua na kutengua wakuu wa vyombo vya usalama kwa mujibu wa katiba na sheria, pamoja na utaratibu wa kubadilisha utaratibu huo. Kutazama video kamili bofya link📷📷 youtube.com/watch?v=Kmy4FE…

Wakili.tv (@wakilitv) 's Twitter Profile Photo

Amesema hayo Rais Samia leo tarehe 30 Mei 2025 wakati akihitimisha mkutano maalum wa CCM uliofanyika jijini Dodoma. Kusikiliza video kamili bofya link 👇👇 youtube.com/watch?v=Pso2k2…