Tanzania Updates ๐น๐ฟ
@TanzaniaUpdates
Follow kupata updates na ripoti mbalimbali za uhakika kuhusu Tanzania.
ID:1668995452035842049
14-06-2023 14:55:19
61 Tweets
13 Followers
18 Following
Treni mpya ya umeme inatarajiwa kuwasili nchini jumanne Machi 26 mwaka huu tayari kwa kuanza kazi mwezi Julai.
Hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa juzi na shirika la reli nchini (TRC) #TanzaniaUpdates
Waziri wa elimu,sayansi na teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa kupitia sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023 ambayo imeanza kutekelezwa January 2024, wenye taaluma ya ualimu wataanza kufanyiwa tathmini ya mitihani ili kupata ajira #TanzaniaUpdates
Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia, Prof Adolf Mkenda amesema kuwa mitaala mipya imeanza mwaka huu ikihusisha ngazi ya darasa la kwanza na la tatu, upande wa sekondari imeanzia kidato cha kwanza na kidato cha tano pamoja na vyuo vya ualimu #TanzaniaUpdates
Rais wa Senegal, MackySall amekubali kufanya mabadiliko ya tarehe ya uchaguzi mkuu kutoka Disemba 15, 2024 hadi Machi 24, 2024 kutokana na maandamano yanayotaka aheshimu muda wake wa kuondoka madarakani #TanzaniaUpdates
Siku ya wanawake husherekewa kila ifikapo Machi 8, ikilenga kutambua jitihada, harakati na mchango wa wanawake duniani #HappyInternationalWomensDay #TanzaniaUpdates
Kampuni ya Asas inayohusika na usambazaji wa maziwa imetunukiwa tuzo ya heshima kwa viwango na ubora kutoka Super Brand East Africa Choice. Tuzo hizo zimetolewa jijini Dar es Salaam #TanzaniaUpdates
Baraza la sanaa,sensa,filamu na utamaduni la Zanzibar (BASSFU) limemfungia msanii wa bongo fleva Zuhura Masoud 'Zuchu' kuendesha shughuli zozote za kisanaa visiwani humo vilevile imepiga marufuku vituo vya redio na TV kucheza kazi zake kwa kipindi cha miezi 6 #TanzaniaUpdates
Serikali nchini Ufaransa ya rais, Emmanuel Macron imeidhinisha sheria ya utoaji mimba kuwa haki ya kikatiba kwa wanawake ambapo watakuwa huru kufanya hivyo pindi wanapojisikia #TanzaniaUpdates
Serikali kupitia naibu waziri wa mambo ya ndani Jumanne Sagini imetoa siku 14 kuondolewa kwa namba za 3D kwenye magari kwani namba hizo hazitengezwi na wakala mwenye kibali kutoka TBS na pia herufi hizo zina ugumu wa kusomeka katika umbali usiopungu mita 100 #TanzaniaUpdates
EPL : Klabu ya Arsenal imeibuka na ushindi mnono wa mabao 6-0 dhidi ya Sheffield United ugenini usiku wa kuamkia leo
Arsenal bado imesalia nafasi ya 3 wakiwa na alama 61 nyuma ya Manchester City na vinara Liverpool kwa tofauti ya alama 2 #TanzaniaUpdates
Nchini Senegal mamia ya waandamanaji wameripotiwa kuendelea kumtaka rais wa nchi hiyo MackSall kufanya uchaguzi mkuu mwezi mmoja kabla ya muda wa urais wake kuisha April 2, 2024 #TanzaniaUpdates
Waziri wa afya Ummy Mwalimu amepiga marufuku vituo binafsi kuwaondoa wodini wagonjwa ambao ni wanachama wa NHIF mara baada ya saa 48 kupita kutolewa kwa taarifa hiyo na vituo hivyo. #TanzaniaUpdates
Kupitia instagram stori mwanamuziki Wizkid ametudokeza juu ya ujio wa albamu yake mpya ikiwa ni miaka miwili tangu alipoachia albamu yake ya 'More Love, Less Ego' #TanzaniaUpdates
Wizara ya afya inayoendeshwa na Hamas inailaumu Israel kufatia vifo vya wapalestina 100 waliokuwa wakisubiri msaada Gaza #TanzaniaUpdates
TANZIA: Rais mstaafu awamu ya pili, Ally Hassan Mwinyi amefariki dunia hospitali jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa saratani ya mapafu
Mwinyi anatarajiwa kuagwa leo saa 8 mchana uwanja wa uhuru #TanzaniaUpdates
Kiungo wa Juventus, Paul Pogba amefungiwa kujihusisha na soka kwa kipindi cha mjaka minne baada ya kugundulika anatumia dawa za kusisimua misuli, kufuatia vipimo vilivyofanyika Agosti 2023 #TanzaniaUpdates
Washukiwa 5 kati ya 6 wanaohisiwa kuhusika na mauaji ya rapper Kiernan Forbes maarufu kama 'AKA' wamefikishwa katika mahakama ya mkazi jijini Durban hii leo kujibu mashtaka #TanzaniaUpdates
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa vyama vya siasa viendlee kufanya shughuli zao kwa uhuru huku akisisitiza kuwa wanaotaka kuandamana wanaruhusiwa na watalindwa #TanzaniaUpdates