Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali
@gcla1895
The Government Chemist Laboratory Authority is the “Legal Referral Laboratory”. Established under the Government Chemist Laboratory Authority Act,No.8,2016.
ID: 1021391361927499776
https://www.gcla.go.tz 23-07-2018 13:47:31
739 Tweet
1,1K Followers
11 Following
Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ofisi ya Kanda ya Kaskazini inaendelea na mafunzo ya siku tatu ya usimamizi salama wa kemikali kwa wadau wa kemikali yanayofanyika katika hoteli ya corrido spring, jijini Arusha.
Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ofisi ya Kanda ya Mashariki imekamilisha Mafunzo ya Mwaka ya Uimarishwaji kwa wasimamizi wa kemikali kwa wadau wa kemikali. yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia Desemba 1 hadi 3, 2025 kwenye ukumbi wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha, Mkoani Pwani.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Adam Malima amewakabidhi zawadi watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali walioibuka washindi katika michuano ya SHIMMUTA 2025.Medali ya Dhahabu kwa Martha Msolla kwa kuwa mshindi wa kwanza mbio za mita 100 kwa wanawake wenye umri wa miaka 50.Kombe kwa Sholastica Hyera
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko na baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wametembelea eneo la ujenzi wa ofisi za Kanda ya Mashariki, Dar es Salaam kuona maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo na kupata maelezo kutoka kwa wakandarasi wa CRJE (East Africa) ltd
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wamefanya ziara ya kutembelea eneo la ujenzi wa mradi wa jengo la Ofisi ya Kanda ya Mashariki ambalo linaendelea kujengwa jijini Dar es Salaam, Desemba 18, 2025.
Wataalam wa Maabara kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wamepata mafunzo ya Utekelezaji wa Mifumo ya Ubora ya Maabara (ISO/IEC 17025:2017) yanayoendelea kufanyika katika Chuo cha Ustawi wa Jamii,Dar es Salaam kuanzia Januari 5 - 9, 2026.Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wataalam hao.
Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kupitia Ofisi ya Kanda ya Ziwa imetoa mafunzo ya matumizi salama ya kemikali kwa wajasiriamali wadogo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa TMDA jijini Mwanza Januari 12, 2026. Zaidi ya wajasiriamali 80 wameshiriki mafunzo hayo ya matumizi salama ya kemikali.